Pages

Tuesday, June 28, 2011

MAONYESHO YA SABASABA YAANZA

Maonyesho ya 35 ya Kimataifa ya Biashara (Tan Trade) sabasaba yameanza leo jijini Dar es Salaam na zaidi ya nch 16 zimeshiriki kushiriki maonyesho hayo.Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Ramadhani Khalfan, amesema maoonyesho hayo yamekuja na tofauti kubwa ambapo amesema viingilio havitabadilika tofauti na miaka ya nyuma

Pia amesema mabadiliko mengidne ni kuweza kuchapisha tiketi za viingilio nje ya nchi ili kudhibiti uharifu wa mapato katika maonyesho hayo

Amesema nchi 17, mashirika binafsi kutoka nchi 28, kampuni zipatazo 300 za nje ya nchi na kampuni zipatazo 1,500 za ndani ya nchi zimethibitisha kushiriki maonyesho hayo

Mabadiliko mengine aliyoainisha ni kupigwa marufuku maonyesho ya muziki ndani ya viwanja hivyo ili kutoa fursa kwa wananchi kupata maelezo mazuri katika mabanda bila kuathiriwa na kelele ya muziki kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Kilele cha maonyesho hayo yanatarajiwa kuwa Julai 7 mwaka huu

No comments:

Post a Comment