Pages

Thursday, March 20, 2014

MITAA YA MWEMBE YANGA

 Mtaa Ngende kwa Msoloboko
 Mwembe Yanga Mchana huu
 Mtaa Mpolwe karibu na soko la stereo
Barabara ya soko la stereo

Monday, March 17, 2014

Kinega; Kijana ‘muuza unga’ aliyepitia misukosuko mingi katika maisha-5

Na Frolence Majani : Mwananchi
Kwa ufupi
  • Wiki iliyopita tuliona jinsi Kinega alivyobuni mbinu mpya ya kuzificha dawa za kulevya alizokuwa akiuza kwenye pipa la taka. Polisi wanafika eneo lake la kazi. Je, Kinega ataepuka kifungo safari hii?

Ghafla polisi walifika eneo lake la biashara na kumkamata yeye na mwanamke wa Kishona kutoka Zimbabwe, aliyekuwa akiuza matunda karibu na alipo yeye.

Polisi waliwakamata na wakahojiwa, lakini kamera zilionyesha kuwa, Kinega alikuwa akienda kwenye pipa la taka mara kwa mara. Polisi walikwenda kwenye pipa na kutoa vifurushi kadhaa vya bangi.

“Nilikuwa na vipisi kama 19 hivi na kama ningeviuza ningepata kiasi kikubwa cha hela, kwa hiyo ikawa hasara kwangu,” anasema kijana huyo.

Siku hiyo Kinega aliamua kukabiliana na polisi, akaingia ndani ya gari, ambalo liliendelea kuzunguka jijini hapo huku Kinega akijaribu kuwaomba wamwachie huru kwa kujaribu kuwapa fedha.

“Tulizunguka kama saa tatu hivi na walipokubali porojo zangu, nikawapa R100, wakaniachia mbele kidogo,” anasema
Hata hivyo, hakukaa sana kabla ya kukamatwa tena kwa mara nyingine na kufungwa kwa miezi miwili jela. Alibahatika kuachiwa huru kwa sababu ushahidi ulikosekana kama mara ya kwanza.

Alipoachiwa mara ya pili, Kinega hakutaka kuuza tena sigara, bali aliuza dawa za kulevya na bangi, lakini kwa kuuchukua mzigo kwa mtu pindi tu mtu anapohitaji na yeye huchukua faida yake (cha juu).

Anajifanya bubu

Siku moja Kinega akiwa kwa mwenyeji wake, simu ilipigwa na Mtanzania mmoja aliyetaka kumpa kazi Kinega.

Wale watu walitaka Kinega aitoe bangi Brii Taxi kwenda kituo kikuu cha treni. Lakini, wakati huo, polisi jamii walikuwa wametawanywa jiji zima la Johannesburg.

Ingawa Kinega alikubali kusafirisha bangi hiyo, lakini alikuwa akihofia sana, lakini aliahidiwa R400.

“Sikuweza kuikataa hiyo pesa, niliomba Mungu anifanyie wepesi katika safari hiyo, nikaanza safari,” anasema Kinega
Alianza safari hiyo huku jiji zima likiwa limetanda polisi jamii waliokuwa wakimkagua kila mtu aliyepita karibu yao.

Kinega akiwa na begi alipiga moyo konde na kuendelea na safari yake. Ghafla polisi mmoja alimshika bega jambo lililomshtua Kinega.

Kinega alipogeuka, akili zilimcheza , akaulizwa unaenda wapi, akaanza kuzungumza mithili ya bubu, polisi yule akamwuliza maswali mengine, lakini Kinega akawa anamjibu ki bubu bubu.

Polisi akamwambia Kinega aondoke akijua kabisa kuwa anazungumza na bubu.

Kinega aliondoka hadi Park Station na kufanikiwa kuukabidhi mzigo kwa mhusika.

Anakutana na mpenzi wa Kihindi

Siku moja Kinega akiwa kwenye treni akielekea Pretoria kwa matembezi, alikutana na msichana mmoja mwenye asili ya Kiasia. Katika treni, Kinega aliketi katika kiti kilichotazamana na msichana huyo.

“Demu (msichana) mwenyewe alionekana ananiangalia sana na mimi nilimtazama sana, kwa kweli wote tulikuwa na hisia za mapenzi, lakini wakati tunakaribia kufika, alikuja kuketi kwenye kiti cha karibu yangu na kuanza kunisemesha Kizulu,” anasimulia Kinega

Binti yule aliyejitambulisha kwa jina la Zaida na hakumficha pale pale akamwambia anampenda kimapenzi.
Huo ulikuwa mwanzo wa Kinega na Zaida, kuwa marafiki, wapenzi ambao walipendana mithili ya kumbikumbi na walifuatana kila mahali kama watoto pacha.

“Wakati huo nilikuwa naishi kwenye vyumba vya bei nafuu ambavyo chumba kimoja kilitumiwa na watu wanne na tulitenganishwa kwa kuweka mapazia,” anasema.

Lakini, Zaida hakujali hilo na alikuja kuishi nami katika chumba hicho cha hali ya chini ingawa alikuwa ni mtoto ambaye familia yake ilikuwa inajiweza.
“Zaida alionyesha kuwa na upendo mkubwa na mimi, alisema anapenda lugha yetu, kwa kweli yule msichana alikipenda Kiswahili hadi akaanza kujifunza,” anasema Kinega

Asingiziwa kubaka

Hakika maisha ni safari yenye misukosuko mingi. Kinega alikuwa amepata mwanamke aliyempenda kwa dhati lakini bado balaa liliendelea kumfuata.

Siku moja wakati Kinega na Zaida wamelala katika chumba cha Kinega, ghafla walisikia hodi na walipomkaribisha mgeni huyo, walishangaa kumwona askari mwenye nyota nyingi na ghafla Zaida alishangaa na kutamka, ‘mama’.

Baadaye, Kinega aligundua kuwa yule alikuwa mama mzazi wa Zaida, ambaye ni polisi mwenye cheo kikubwa jijini Johannesburg.

Mama yule alimhoji binti yake maswali kadhaa ikiwamo kwa nini anaishi kwenye nyumba chakavu namna hiyo? Zaida alisema ni kwa sababu anampenda mpenzi wake Mtanzania, Kinega.

“Mama yake Zaida, alituambia anataka tuhame kwenye nyumba hiyo mara moja na hivyo alituahidi kututafutia nyumba siku yeyote kuanzia siku hiyo,” anasema.
Baada ya siku chache, Zaida na Kinega walihamia kwenye nyumba waliyotafutiwa na mama yake Zaida. Ilikuwa furaha kwa Kinega na huo ukawa mwanzo wa maisha mapya kati ya wawili hao.

Siku moja Kinega na Zaida wakiwa wamepumzika kwenye bustani moja jijini humo, walitaniwa na kijana mmoja wa Kitanzania aliyewaambia, nyinyi mbona mnamwacha Mtanzania mwenzenu analala majalalani?

“Yule kijana alituonyesha kwa mbali mtu akiwa amelala kwenye daraja na amejifunika makasha chakavu. Tulinyanyuka na tukamsogelea. Kweli alikuwa ni Mtanzania” anasema

Anasema baada ya kumfahamu Mtanzania huyo, Zaida alishauri wamchukue na kuishi naye kwenye nyumba yao. Jambo ambalo Kinega alikubali kumsaidia kwa sababu hata yeye alisaidiwa alipofika Johannesburg.

Kinega alimsaidia Mtanzania huyo (jina linahifadhiwa) na wakaanza kuishi pamoja kwa kutenganisha vyumba na pazia kama ilivyo ada kwa wenyeji wa hapo.
Baada ya miezi sita, Mtanzania huyo naye alifundishwa kufanya biashara na kwa bahati nzuri, alipata mwenza wa kabila la Kizulu, aitwaye Sibonile.

“Yule msichana alikuwa anakuja na kuondoka, lakini baadaye, akahamia kabisa pale tulipokuwa tunaishi na kwa kuwa Zaida alikuwa na roho nzuri, aliwaruhusu tuishi nao,” anasema. Siku moja usiku wa manane wakiwa wamelala, Kinega alisikia sauti kali za watu wakigombana. Sauti hizo zilikuwa ni za yule mgeni wa Kitanzania na mpenzi wake, Sibonile.

Kinega alipokwenda chumbani kwao kuhoji kulikoni, aliwakuta wanavuta dawa za kulevya na kumbe hicho ndicho chanzo cha ugomvi wao.

“Niliamua kuwafukuza kwa sababu wamenivunjia heshima halafu waliniudhi wao kuvutia dawa za kulevya ndani tena kwenye nyumba waliyokaribishwa,” anasema.

Kitendo cha Kinega kuwafukuza, kilimuuchi mno Sibonile ambaye alimwambia Kinega kwa lugha ya Kizulu kuwa, ‘utaona wewe mkimbizi, utaona’.

Siku kadhaa zilipita na siku moja asubuhi Kinega na Zaida wakiwa wamejipumzisha, walisikia mtu akibisha hodi, kabla hata ya kufungua, walishangaa kuona kundi la askari likiingia ndani.
“Polisi walinikamata wakati huo sijui kosa nililofanya, lakini mpenzi wangu alikuwa akilia na mpaka alijaribu kupigana na wale askari,” anasema.

Kinega aliswekwa rumande na kupewa kikaratasi chake cha mashtaka, bila kukisoma, alielekea mahabusu na kujilaza na hata baadaye alipokisoma kikaratasi alichopewa, ndipo alipogundua kuwa anashtakiwa kwa kesi ya ubakaji.

“Nililia sana, yaani nililia kwa sababu nilijua kabisa kuwa, kwa kesi hiyo na mimi ni mgeni nitaozea jela, kwa kweli iliniuma kwani nilikuja kugundua kuwa, Sibonile ndiye aliyenitengenezea hiyo kesi,” anasema

Kinega aliendelea kukaa mahabusu kwa muda mrefu huku kesi yake ikiendelea kusomwa, ingawa hakutakiwa kujibu lolote kwani alipewa mwanasheria wa Serikali aliyekuwa akimtetea.

“Kila siku ambazo kesi yangu ilikuwa inasomwa, Zaida alikuwa anakuja mahakamani na kuniletea nguo, nguo za ndani, sabuni, mafuta na vyakula, yaani alitumia gharama kubwa sana na alikuwa analia akiniangalia,” anasema.

Aliendelea kusota jela kwa muda mrefu hadi siku moja, mwanasheria wake, alipowatuma maofisa upelelezi kwenda kuchunguza kwa kina kesi ya Kinega katika makazi aliyokuwa anaishi.

MABADILIKO YA YOMBO BUZA

 Mzunguko wa Yombo Buza kwa Mama Meri


 Kilima cha kuelekea Buza
 Maeneo ya Abiola


Davis Corner ilivyo sasa

MVUA KIDOGO TEMEKE YETU TAABANI

 Hii ni mifereji ambayo imeziba na kusababisha maji yasiwe na njia ya kupita

 Barabara maji matupu

Baadhi ya mitaa ilivyo maeneo ya temeke kwa sasa kipindi cha mvua