Pages

Friday, November 6, 2015

JAJI MASAJU AAPISHWA IKULU



Raisi wa awamu ya tano Dr.John Magufuli amemuapisha rasmi leo mwanasheria mkuu wa serikali jaji Masaju

Tuesday, October 13, 2015

AVAMIA KITUO CHA POLISI NA PANGA




HALI tete! Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke, Dar lilifanikiwa kumdhibiti mtu mmoja ambaye jina lake halikupatikana mara moja kufuatia madai ya kuvamia Kituo cha Polisi Charambe akiwa na panga.


Habari zilizopatikana kutoka kwa raia wa eneo hilo ambao walimtafsiri mtu huyo kama gaidi kutokana na ujasiri wake wa kuvamia kituo kwa mapanga kwa lengo la kutaka kuwajeruhi askari kituoni hapo bila uoga.


Uwazi ambalo lilifika kituoni hapo mara baada ya tukio hilo, liliambiwa kwamba mtu huyo alijitokeza kituoni hapo majira ya saa sita mchana na kuanza kuwapiga polisi na ubapa wa panga hali iliyozua tafrani.


Wananchi hao kwa nyakati tofauti walisema kwamba, mtu huyo alikuwa na nguvu nyingi kiasi cha kuwafanya askari kuchukua muda mrefu kumdhibiti kwani hapa kumpiga pingu ilikuwa shughuli pevu.


Taarifa zaidi toka kwa wananchi hao zinadai kwamba, ili askari waweze kumdhibiti ilibidi afungwe pingu haraka. Hata hivyo, licha ya kujeruhiwa miguu bado alikuwa akiongea kwa sauti ya juu nje ya kituo hicho, akiwalaani askari hali iliyowafanya wananchi kuzidi kujaa huku wakidai si mtu wa kawaida.


Vyanzo vingine makini vilidai kwamba, kutokana na hali iliyojitokeza kwa mtu huyo kutotii amri ya polisi iliwafanya askari waongezeke baada ya kupigiwa simu kwa hofu kuwa huenda ana wafuasi wake ambao wangeweza kuvamia kituo wakati wowote.

Vyanzao hivyo viliendelea kudai kwamba zaidi ya difenda tatu ambazo zilikuwa na polisi zilifika kituoni hapo muda mfupi baadaye na kila askari alionekana akiwa tayari kwa lolote.


Ilidaiwa kwamba hali hiyo ilimfanya Kamanda wa Polisi Temeke, ACP Andrew Satta kufika ili kushuhudia hali hiyo kwa macho.

Baadhi ya wananchi walisema mtu huyo alikuwa na wenzake ambao haikujulikana walikoelekea na ndiyo sababu polisi walipatwa na hofu. Mtu huyo alichukuliwa hadi Kituo cha Polisi Mbagala kwa mahojiano zaidi.


Kamanda Satta alipohojiwa na Uwazi kwa njia ya simu alisema hayupo ofisini hivyo alimtaka mwandishi kufika ofisini kwake. Mwandishi alipofika hakumkuta ofisini na simu yake ilipopigwa ilikuwa ikiita bila kupokelewa.


Bado gazeti hili linaendelea kufuatilia suala hilo kwa karibu ili kujua ni kitu gani kilitokea.

Chanzo: GPL

Wednesday, September 9, 2015

Friday, September 4, 2015

GARI YA MBUNGE YAPATA AJALI



Mgombea ubunge katika jimbo la kisarawe Kingwendu amepata ajali maeneo ya kisarawe alipokuwa katika harakati za kampeni ila hakuna aliyeumia katika ajali hiyo

Thursday, August 27, 2015

MOTO WATEKETEZA WATU TISA BUGURUNI





Nyumba moja maeneo ya buguruni imeteketea kwa moto na kusababisha watu 9 wa familia moja Kufariki, mpaka sasa haijajulikana chanzo cha moto huo ulikuwa nini.

Monday, August 17, 2015

MANJI AFUNGUKA KUKATWA KWAKE



Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji ambaye amekatwa kuwania udiwani Mbagala Kuu, amesema alikuwa ni mgonjwa.


Manji ambaye ameshinda kwa kura nyingi katika kura za maoni, lakini akaenguliwa kwa madai hakuwa katika eneo husika, imesababisha kuzua hasira kwa wananchi wa eneo hilo.

Jana wananchi hao walifika katika Makao Makuu ya CCM jijini Dar es Salaam wakitaka kujua hatma ya Manji.

Wengi walihoji kwamba Manji amekatwa kwa fitna zinazozihusisha Yanga na Simba ambazo ni klabu kongwe za soka nchini.

“Nilikuwa mgonjwa, inajulikana. Hali yangu haikuwa nzuri, hivyo nisingeweza kufika,” alisema Manji alipozungumza na SALEHJEMBE.

Hata hivyo Manji alisisitiza, asingependa kulizungumzia suala hilo kwa kuwa bado linasikilizwa ndani ya chama.


“Nafikiri tuache kwanza, subira ni jambo zuri

BASI ZA MWENDO KASI ZAZINDULIWA LEO DAR



WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia amewataka madereva wanaofanyiwa mafunzo ya kutumia mabasi yaendayo kasi kuyazingatia ili kuwa na ufanisi mzuri wa kazi. Anaandika Hamisi Mguta … (endelea).
Amesema hayo katika uzinduzi wa mafunzo ya uongozaji wa mabasi yaendayo kasi chini ya Kampuni ya UDART kwa madereva uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Ghasia amesema katika kipindi hiki cha mafunzo ya utumiaji wa mabasi ya haraka, hakutakuwa na mfumo kamili wa matumizi uliopangwa kutumika katika mabasi hayo na kwamba, kutakuwa na kamera ndani ya mabasi hayo zitakazoweza kuonesha kinachoendelea ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za dharura.
Aidha amewataka watakaofanya kazi ya kuhudumia abiria ndani ya mabasi hayo kuwa wakarimu kwa abiria ili wafike katika vituo vyao kwa usalama na furaha zaidi.
“Tanzania ni nchi ya pili barani Afrika ikiongozwa na Afrika Kusini kutumia mabasi yaendayo haraka na tunatarajia kuwa na mafaniko zaidi ya Afrika Kusini.”
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Saidi Meck Sadiki amewataka wananchi kuzingatia na kusimamia miundombinu ya mabasi hayo kuepuka kuchakaa mapema.
Amesema mabasi hayo yenye uwezo wa kubeba watu hadi 500,000 kwa nusu saa yatafanyiwa mafunzo kwa madereva chini ya uongozi wa VETA (Chang’ombe) ili kuleta ufanisi mzuri wa kazi.
Mwakilishi kutoka VETA, Samwel Nganya amesema madereva watakaoendesha mabasi hayo ni wale watakapewa leseni za kimataifa na watakuwa na uwezo wa kufanya kila kitu peke yao pasipo na konda kwani mabasi hayo yanaongozwa na dereva tu.
Nganya ameongeza kuwa, madereva wanaohitajika ni 330 lakini madereva 149 ndio waliopatikana kwa majaribio ya vitendo, hivyo bado kuna uhitaji wa madereva 181 zaidi kufikia idadi kamili.
Licha ya kuwapa mafunzo madereva hao Nganya amesema, wana mpango wa kutoa mafunzo mahususi hasa kwa wahudumu wa wateja (customer care) kuhakikisha huduma zinakwenda sawa.

Sunday, August 16, 2015

MANJI AKATWA UDIWANI MBAGALA KUU


YUSUF MANJI Akatwa UDIWANI MBAGALA!!!


YUSUF MANJI akatwa UDIWANI MBAGALA!!!
VURUGU kubwa zimetokea katika ofisi ya CCM mkoa wa Dar es Salaam baada ya Wanachama wa chama hicho, kupinga hatua ya uongozi wa CCM mkoani hapa kutengua ushindi wa kura ya maoni kwenye ngazi ya Udiwani kata ya Mbagala kuu aliopata Yusuf Manji, ushindi huo kupatiwa na aliyeshika nafasi ya pili katika ngazi hiyo Abubakari Athumani.Anaandika KAROLI VINSENT

TAMASHA LA DEMOKRASIA MBAGALA ZAKHEIM




Tamasha la democrasia Leo viwanja vya mbagala zakheim

Monday, August 10, 2015

KANUSHO KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAISI


MH. LOWASSA ACHUKUWA FOMU YA URAISI

 Baadhi ya watu waliojitokeza kumsindikiza Mh.Lowassa leo
 Barabara zote za kuingia mjini zilikuwa hazipitiki



hali mpaka sasa hivi shwari na Lowassa keshakabidhiwa fomu rasmi