Pages

Thursday, October 23, 2014

MKE AKIRI KUMSALITI MUMEWE MIAKA 7

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya kulawiti na kutuma picha katika mitandao ya kijamii inayowakabili wakazi wawili wa Mbagala, Dar es Salaam, alidai kwamba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mlalamikaji kwa miaka saba huku akiwa na mume wake ambaye ni mshitakiwa namba moja katika kesi hiyo.
Sanifa Sadick alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi Saidi Mkasiwa kuwa mshitakiwa Erick Kasira (39) ni mume wake tangu mwaka 2006 na kwamba wana watoto wawili huku mshitakiwa wa pili, Juma Richard ni shemeji yake.
Alidai kwamba Agosti 23 mwaka huu, waliwasiliana na mlalamikaji huyo ili wakutane katika nyumba ya kulala wageni inayojulikana kama Maembe Bar & Guest House iliyopo Yombo Kiwalani kwa ahadi ya kusaidiwa Sh 100,000.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Sylvia Mitanto, shahidi huyo alidai muda wa saa 7 mchana alimuaga mume wake kwamba anaenda kununua bidhaa za saluni.
Alidai kwamba alichukua usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda huku mlalamikaji akimuelekeza kwa njia ya simu.
Sanifa alidai kwamba wakati anaelekea Yombo kulikuwa na mwendesha pikipiki ambaye alikuwa anamfuatilia kwa nyuma hadi eneo hilo.
Alidai kwamba alimkuta mlalamikaji akiwa peke yake na kuagiza kinywaji baadaye walichukua chumba namba sita na kuingia ndani; baada ya muda mlango wa chumba hicho uligonjwa ndipo alimuona mumewe akiingia pamoja na vijana watatu.
‘’Sikuweza kuwatambua wote lakini hawakuwa na silaha zaidi ya simu. Mpenzi wangu aliulizwa na mume wangu kuwa anafanya nini na mimi, naye alimjibu kuwa asiniache kwani atampa gharama yoyote ndipo waliandikishiana kutoa Sh 500,000 ,’’ alidai Sanifa.
Alieleza mlalamikaji kuwa alikuwa na kompyuta na kwamba alimwambia Erick akae nayo hadi atakapompatia fedha hizo walizoahidiana.
Alidai kwamba alikuwa amejificha chooni na kusikia kwamba wanaume hao wanamtaka mlalamikaji afanyiwe kinyume na maumbile na kwamba walimvua nguo zote huku aliyekuwa mwendesha bodaboda akiwa anapiga picha.
Alidai baada ya tukio hilo alikimbilia nyumbani na kukuta simu aina ya Tecno nyumbani kwake na kuiweka laini yake baadaye dada yake alimtumia picha ikimuonesha mlalamikaji akiwa utupu.
Alieleza kwamba mlalamikaji alimpigia simu Erick na kumwambia aende akachukue fedha alizoahidi kutoa wakati akifumaniwa na mke wa mshitakiwa huyo na kwamba mshitakiwa huyo aliondoka pamoja na ndugu yake Richard.

Alidai walipofika Tandika, waliwekwa chini ya ulinzi na Erick alimpigia simu mkewe kumtaarifu kwamba amekamatwa na polisi naye alipofika aliwekwa chini ya ulinzi. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 3 mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa.

CHANZO: Habari Leo

BASATA KUMVUA TAJI MISS TZ 2014

Sakata la lililojitokeza la mrembo wa Taifa wa mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2014', Sitti Mtemvu kudaiwa kudanganya umri, limeingia katika sura mpya baada ya Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kueleza kuwa litamvua taji hilo endapo itabainika kweli alichakachua umri wake.

Katibu Mkuu wa Basata, Geoffrey Mwingereza, aliliambia NIPASHE jana kuwa baraza hilo linasubiri uchunguzi ukamilike na endapo watabaini kuna udanganyifu ulifanyika hawatakuwa na la kufanya zaidi ya kumvua taji.

Wakati Mwingereza akieleza hayo, viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wanatarajia kukutana leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili sakata hilo la Sitti.

Akizungumza na NIPASHE jana, Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia, alisema serikali imesikia taarifa za mkanganyiko kuhusiana na mrembo huyo hivyo imeamua kuitisha kikao ili kuanza kulifanyia kazi.

Nkamia alisema kamwe serikali haiwezi kukaa kimya pale ambapo jina la nchi linatajwa vibaya.

"Siwezi kukuambia hatua gani zitachukuliwa, ila kesho (leo) tutakuwa na kikao, serikali haiwezi kukaa kimya, kuna vyombo vyake vinalifanyia kazi," alisema Naibu Waziri huyo.

Aliongeza kuwa yeye alikuwa nje ya Dar es Salaam, lakini tayari kuna maelekezo aliyoyatoa na yameanza kufanyiwa kazi na wizara hiyo.

Siku moja baada ya Sitti kutangazwa mshindi wa taji hilo, taarifa za mrembo huyo kuhusu umri wake zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa ana miaka 25, hivyo hana sifa za kushiriki shindano hilo hapa nchini.

Nakala ya hati ya kusafiria ya mrembo huyo ambayo ilitolewa Februari 15, 2007 na muda wake wa kumaliza kutumika ukiwa ni Februari 14, 2017 yenye namba AB 202696 inaonesha Sitti ambaye pia anashikilia taji la Kitongoji cha Chang'ombe na Kanda ya Temeke, alizaliwa Mei 31, 1989.Pia taarifa nyingine zinazoone sha mrembo huyo ana miaka 25 ni zilizokuwa kwenye Taasisi ya Explore Talent, ikimtaja kwamba anaishi Dallas, Texas, urefu wake ni 5'8, umbo lake ni la kati, asili yake ni Mwafrika na rangi ya macho yake ni kahawia.

Juzi, Kamati ya Miss Tanzania iliyoko chini ya Mratibu wa shindano hilo, Hashim Lundenga, ilisema kuwa Sitti amezaliwa Mei 31, 1991 katika wilaya ya Temeke jijini kwa mujibu wa cheti chake cha kuzaliwa alichokionesha.

Lundenga alionesha cheti cha kuzaliwa cha Sitti ambacho kimetolewa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Septemba 9, mwaka huu kikiwa na namba 1000580309 na kikimtaja baba yake ni Abbas Mtemvu Zuberi (Mbunge- Temeke) wakati mama ni Mariam Nassor Juma (Diwani- Temeke).

Hata hivyo, Lundenga alisema kuwa kamati yake inaendelea na uchunguzi kuhusiana na taarifa hizo na endapo watabaini kuwepo na udanganyifu watamchukulia hatua mrembo huyo kwa kushirikiana na Basata.

Pia Lundenga na Sitti, walikanusha taarifa za mrembo kuwa kuwa na mtoto na kusema kwamba mwenye uthibitisho wa jambo hilo anatakiwa aliwasilishe kwa kamati ili hatua zichukuliwe.

Sitti aliibuka kidedea katika shindano la urembo la taifa lililofanyika usiku wa Jumamosi ya Oktoba 11 kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini na kuwashinda washiriki wenzake 29 waliokuwa wanawania taji hilo.

CHANZO: NIPASHE

Wednesday, October 22, 2014

KAPUMZIKE KWA AMANI YESAYA AMBOKILE YP

 Mwili wa marehemu ukitolewa Temeke Hospital
 Juma Nature, KR na Dolo walikuwepo kumsindikiza ndugu yao YP
 Madee, Fella na Chege wakisubiri kuushusha mwili wa marehemu nyumbani kwao keko
 Temba, stiko na Martin
 watu wakipata chakula

 Jeneza la marehemu likisubiri ibada ya mwisho
 Mchungaji akitoa nasaha zake


 Mkubwa fella akienda kutoa historia fupi ya marehemu


 Mwili wa marehemu ukipelekwa viwanja vya sigara kuagwa



 Wananchi waliojitokeza kuaga
 hali ilivyokuwa makaburini
Profesa jay mmoja waliohudhuria katika msiba huo

Sunday, October 19, 2014

NASH MC AFUNIKA TEMEKE SHOW


 Msanii wa hip hop Nash Mc aka Mpish mkuu, kenyata, shokoshugi, maalim nash,vitasamoto ameweza kuwapa burudani ya kutosha wapenzi wake waliofika katika uwanja wa chuo cha Bandari Tandika kwa shoo kali ambayo kila mtu ameondoka akiwa ameridhika na alichokipata
 Tamaduni Muzik walikuwepo
 Ume Masim na Escober wakiwakilisha

 LWP wakitumbuiza
 Snota
 Nash Mc mpishi Mkuu akifanya yake jukwaani







Saturday, October 18, 2014

SIMBA NA YANGA ZASHINDWA KUTAMBIANA

 Foleni ikianzia uwanja wa zamani wa uhuru
 Wafanyabiashara wakiendelea na shughuli zao
 Washabiki waliohudhuria katika pambano hilo ambalo mpaka mwisho matokeo 0-0









MAANDALIZI: NASH MC TEMEKE SHOW

 Hatua ya mwisho ya maandalizi ya Nash Mc Temeke Show itakayofanyika siku ya jumapili ya tarehe 19/10/2014 katika ukumbi wa Bandari kuanzia saa 9 Alasiri
 LWP watakuwepo
 Salii Teknik
 P the MC akibadilishana mawazo na teknik
Nash Mc akiwa na P the Emcee