Pages

Wednesday, July 17, 2013

Timu ya Al Qyadiria ya Mtaa wa Changani Temeke yaikung'uta kwa taaaaaabu 4-0 timu ya Taifa Academy. Pambano lilifanyika kwenye Uwanja wa Skwadi Temeke.


Mchezaji wa timu ya Al Qyadiria ambaye ni mfungaji wa Goli la tatu katika mechi yao na Taifa Academy.


Kocha wa timu ya Al Qyadiria Rajabu Kiazi almaarufu "Ticha" mwenye fulana nyeupe akiwa anaongea kwa kujiamini na baadhi ya Mashabiki wapenda soka. Kutoka kushoto Fadhil Aziz Zinzoo " Mbuyu Twite" ambaye ni meneja wa PUB ya CCM kata ya 15 iliyopo Temeke maeneo ya makutano ya mtaa wa Himo na Kitomondo na mwenye flana ya kibluu ni Godwin Nasser " Mzee wa Utelezi au Gololi" akipeana mikono na Kocha Ticha wa Al Qyadiria ya Temeke. Wengine kwenye picha hiyo ni Mashabiki waliohudhuria mchezo huo Uwanja wa Skwadi.


Wachezaji wa timu za Al Qyadiria na Taifa Academy wakiwa Uwanjani kwenye mechi baina yao ambao Taifa ilikung'utwa goli nne kwa nunge na timu ya Qyadiria.


Beki wa timu ya Taifa Academy akipiga mpira kuondoa moja ya hatari zilizoelekezwa langoni mwake.


Wachezaji wa Qyadiria na Taifa Academy wakipambana vilivyo kwenye mechi baina ya timu zao.


Ama kweli mpambano ulikuwa mkali sana hali iliyopelekea timu ya Al qyadiria kuibuka kidedea kwa taabu sana baina yake na timu ya Taifa Academy leo kwenye Uwanja wa Skwadi Temeke.