Pages

Wednesday, July 17, 2013

Mbunge wa Temeke Mh. Zubery Mtemvu atoa 200,000/= kwa timu mbili zilizoingia Fainali ya Kombe la Diwani kata ya Azimio. Bingwa alichukua zawadi ya mbuzi.

Fainali ilikuwa kati ya timu ya CCM Mji Mpya na Azimio Kaskazini. Bingwa ilikuwa timu ya CCM Mji Mpya kwa ushindi wa penati 7-6 ambapo Diwani wa Kata ya Azimio temeke aliikabidhi timu ya Mji Mpya Mbuzi mnono.

Mgeni rasmi katika Pambano hilo alikuwa mbunge wa Temeke Mhe. Zubery Mtemvu ambapo kwa utashi wake alitoa laki mbili yaani kila timu ilipata laki 1.

MechI zote zilifanyika Uwanja wa Mashine Ya Maji eneo linaloitwa AZIMIO.



Timu ya Mji Mpya CCM ambo ndio walikuwa mabingwa wa Kombe la Diwani kwa kuibuka na kitita cha Laki moja na Mbuzi mnono.


Nyomi ya maana kwenye Uwanja Mashine ya Maji Azimio. Hii ilikuwa mechi ya fainali kati ya Mji Mpya na Azimio Kaskazini.


Mbunge wa Temeke Zubery Mtemvu akiikagua timu ya CCM Mji Mpya huku akiongozwa na mratibu wa mashindano hayo Bw. Albino Lwila.



Mtemvu akifurahi pamoja na viongozi wa CCM waalikwa kwenye pambano la fainali kati ya Mji Mpya CCM na Azimio kaskazini kwenye Uwanja wa Mashine ya maji Azimio Temeke.