Pages

Sunday, July 7, 2013

HISIA ZA MTOTO WA TEMEKE NATAMASHA LA MATUMAINI

Shigongo pamoja na timu nzima mlioandaa huu mpango mnazingua mazima kwa kuzidi kujitajilisha kupitia tamasha mliloandaa wenyewe huku Shigongo ukitumia kauli mbiu yako "kufeli shule sio kufeli maisha" kakudanganya nani katika dunia ya leo inayotaka elimu na pesa kama huna elimu kuwa na pesa. Pesa ndio inaleta elimu bora kwa sasa. Ikiwa kweli umeamua kusaidia elimu ya Tanzania... haikuwa na haja ya kutoa asilimia 10 ya mapato yatakayopatikana apo mlangoni siku ya tamasha, kwani watanzania watakaoingia apo ni zaidi ya asilimia kumi unayotoa wewe kupeleka kwenye elimu sasa hzo asilimia nyingine 90 zinaenda wapi na kufanya nini au ndio zinaenda kutafuta matukio ya kudhalilisha watanzania kupitia magazeti yako yanayoandika habari za uzushi, uongo, kuwagombanisha watu na familia zao kuwafanya waonekane wajinga katika jamii ya watanzania wanaosoma magazeti yako uliyoyabatiza jina jipa "magazeti pendwa" huku ukijua kinachoandikwa ni udaku pakiwa na neno "habari na mwandishi wetu" hv huyo mwandish wenu hana jina au ndio jina lililopa ajira ni "mwandishi wetu" habari ikiwa za kweli lazima jina la mwandish aliyekuwepo eneo la tukio liwepo. Kwa upande wangu mimi naona haikuwa na haja ya kudanganya watanzania kupitia matatizo ya elimu yetu kuwa unawasaidia kwa asilimia 10 ikiwa asilimia 90 ujasema zinapoenda, ni hv ungetumia tu pesa ya magazeti yako uliyoyaita pendwa kuchangia asilimia kumi uliyochagua wewe na wasomaji wengi wa magazeti yako ni wanafunzi na wao ndio wahusika wakuu wa kuchangiwa huo mchango tamasha lako ungeliandaa kwa mengine kabisa unayoyajua wewe na mafisadi wenzako mliojificha kwenye ulokole.

Pia wabunge nyie ndio wanafiki wakubwa katika elimu yetu mliwah kukataa hoja ya mh flani mkisema elimu haina tatizo mpaka matokeo mabovu yakawaumbua. Nyie mngetumia posho ya kikao kimoja kuchangia katika elimu ingetosha sana kuliko kuja kusapoti wizi wa akili kama huu uliopewa jina tamasha la matumaini. Tambueni kwenye njaa na dhiki apaponywi kwa mkate mkavu. Elimu yetu inaitaji mchango mkubwa sana sio huo wenu mnaofanya sasa wa kimagumashi kuboresha miladi yenu.


Mwana Hisia Tmk
Dee Dion