Pages

Monday, July 15, 2013

Kombe la Diwani kata ya Miburani bado linaendelea. Ngeta na Mwarobaini zatoka sare ya 3-3.

Mwita, Humud Mwarabu na baadhi ya mashabiki wa timu ya Mwarobaini wakifuatilia mchezo kwa undani kabisa kwenye uwanja wa Temeke Squad Temeke leo jijini Dar es Salaam.

Mwamuzi wa mchezo wa leo kati ya Ngeta na Mwarobaini aakimuelekeza mchezaji wa Ngeta Mabruki sehemu sahihi ya kuweka mpira kabla ya kuupiga. Mechi iliisha kwa sare ya 3-3.

Mchezaji wa Ngeta Mabruki akipiga mpira wa adhabu kuelekea kwenye lango la Mwarobaini leo.

Kocha wa Mwarobaini Habib Sultan a.k.a Pep Guardiola  na Mkurugenzi wa timu ya Mwarobaini 
 Bw. Maliki wakitoa mawaidha kwa wachezaji wao wakati wa mapumziko leo jioni mechi iliisha kwa sare.

Mwenyekiti wa Tawil la CCM kata ya 15 Wailes Temeke jijini Dar es Salaam Bw. Asad Mfaume mwenye suti nyeusi akifuatilia kwa makini mawaidha yanayotolewa na kocha wa Mwarbaini.

Wachezaji wa Ngeta na Mwarobaini wakiwa mchezoni Uwanja wa TMK Squad leo Temeke.