Pages

Monday, August 6, 2012

Laylatul Qadir (Usiku wa Cheo)

Asalaam Alaykum Warahmatu llahi Wabarakatu 

Ama Baada ya Salamu naomba Toa Shukran zangu za Dhati  Timu Nzima ya Blog hii ya Jamii Japo Nimechelewa kuwatakia Kheri ya Mfungo wa Mwezi wa Ramadhani Wadau wote pamoja na Timu yako Naomba Pokea Salamu zangu na Tunamuomba M/Mungu azipokee Funga Zetu na Dua zetu kwa Ujumla.

Naomba Nita barouk kidogo ( Tupate barka )  kwa Pamoja kwa kukumbushana Siku hii Muhimu katika Siku ambazo Ndio zimeufanya Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani kuwa Mwezi Mtukufu  nayo Ni Siku ya LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO).

LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO) NI USIKU AMBAO 

UNAPATIKANA NDANI YA MWEZI HUU MTUKUFU WA 

RAMADHANI NDANI YA KUMI LA MWISHO MTUME (S.A.W) 

LILIPOKUWA LIKIINGIA KUMI LA MWISHO ALIKUWA 

AKIZIDISHA IBADA KWA SANA NA KUWA AMSHA WATU 

WAKE ( ALHAL BAYTI ) KWA AJILI YA KUFANYA IBADA 

ZAIDI KATIKA KUMI HILO.

LAYLATU QADIR SI MWEZI 27 TU ILA WENGI WA 

WANACHUONI WAMEJITAHIDI KUWA HIYO NDIO SIKU YA 

LAYLATUL QADIR 

SIKU HII INAPATIKANA NDANI YA  MWEZI 21 , 23 , 25 , 27 , 

29 , NI JUU YETU NDUGU ZANGU KUITAFUTA SIKU HII 

KWA KUFANYA 

IBADA KWA WINGI NDANI YA KUMI LA 

MWISHO ILI M/MUNGU ATUWEZESHE KUIDIRIKI SIKU 
AMBAYO UBORA WAKE NI ZAIDI YA MIEZI 1000 NA 
HUSHUKA MALAIKA NDANI YA SIKU HIYO KWA IDHINI YA 
M/MUNGU SUBHANAHU WATAALAAH .

UTUFUKU WA SIKU HII NI UNAPATIKANA KWA MAMBO 
MAKUU MAWILI KUTEREMKA KWA QUR AN ( MUNGOZO 
WA MUISLAM)

KUSHUKA KWA MALAIKA KWA IDHINI YA MOLA MTUKUFU.

NA IBADA YA SIKU HII UBORA WAKE NI ZAIDI YA MIEZI 
1000.

 NI JUU YETU KUHAMASISHANA NAKUKUMBUSHANA 
KUWA SIKU HII SI SIKU MOJA NA MUHIMU SANA ILI 
KUPATA KUMUOMBA MUNGU NA KULIOMBEA TAIFA LETU 
NCHI YETU YA TANZANIA MUNGU KULIPA BARKA.

SIKU HII MUNGU AKIKUBARIKI KUIDIRIKI DUA YA 
KUOMBA 
NI HII KWA MAELEKEZO YA MAMA AISHA 
alimuliza Mtume 
Jee? tukiidiriki LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO) tufanye 
nini ? Mtume akajibu kithrisha kusema NASH-HADU ANLAA 
ILAAHA ILLA ALLAHU NASTAGHFIRULLAH NAS'ALUKAL 
JANNATA ILAAHI WANAUDHUBIKA MINA NNAAR 
ALLAHUMA INNAKA AFUWUN TUHIBUL AFWAA 
FA'AFUANNAA YAA KARIYMAL AFWU ". Kama alivyosema Mtume

MUNGU NDIYE MJUZI WA HII SIKU LAKINI INAPATIKANA 
NDANI YA KUMI LA MWISHO LA RAMADHANI.


Ghalib N Monero.
Al- Azhar University 
Cairo Misri

No comments:

Post a Comment