Pages

Wednesday, February 2, 2011

TAMASHA LA MASKAUTI -TEMEKE


Chama cha Maskauti wilaya ya Temeke inawatangazia Tamasha la Maskauti litakakalofanyika kwenye viwanja vya maonyesho ya Sabasaba vilivyopo wilayani Temeke kuanzia tarehe 18/02/2011 hadi tarehe 20/02/2012.

Madhumuni makubwa ya Tamasha hilo ni:-
  1. Kuazimisha siku ya skauti duniani kwa kumbukumbu mwanzilishi wa skauti Sir. Robert Baden Powell.
  2. Kukuza vipaji vya skauti/wanafunzi kwa kufanya mashindano ya michezo mbalimbali ya kunoa akili na ya kuchangamsha mwili.
  3. Kumwandaa kijana kuwa na tabia nzuri inayofaa kwa jamii.
  4. Kuwakaribisha skauti wapya
Ili kijana wetu aweze kushiriki katika tamasha hili la kuelimisha na kukuza vipaji 
wasiliana kwa namba zifuatazo :
  • 0657 202983
  • 0759 364187

No comments:

Post a Comment