Pages

Sunday, April 29, 2012

SIMBA YA ULAYA


 Nyomi iliyofulika kuja kuangalia mechi


Mchezaji wa timu ya Simba Mganda Emmanuel Okwi akikokota mpira kuelekea goli la timu ya Al Ahly Shandy, huku mchezaji wa timu ya Isaac Seun Malik wa timu ya Al- Shandy ya Sudan akijaribu kumzuia katika mchezo wa kombe la Shirikisho unaofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam Simba, imefanikiwa kuitandika Al Shandy ya Sudan magoli 3-0 katika kipindi cha lala salama na kutoka kifua mbele katika mchezo huo wa kwanza kabla ya ule wa Sudan wiki mbili zijazo.
Magoli ya Simba yamefungwa na wachezaji Haruna Moshi dk 66, Patrick Mafisango dk 77,  na Emmanuel Okwi88, hata hivyo mchezji Patrick Mafisango alikosa penati baada ya mchezaji Emmanuel Okwi kuchezewa vibaya na beki wa timu ya Al Ahly Shandy katika kipindi cha kwanza.

No comments:

Post a Comment