Pages

Monday, June 4, 2012

MATESO YAMEMZIDI

UKISTAAJABU YA MUSA....NILIYOYAKUTA KWA SHABANI H.KALEMBO
RUKIA ABDALHA ni mtoto wa miaka miwili anayeishi RUANGWA(LUGALO) mkoani LINDI aliungua maji ya moto,akapelekwa hospitali ya wilaya RUANGWA ambako alipata huduma ya kwanza na kushauriwa aende NDANDA,NYANGAO au MUHIMBILI.Wazazi wa RUKIA hawana uwezo kifedha kumfikisha ktk hospitali hizo,wanazidi kumuuguza mtoto huyo kienyeji nyumbani kwao na sasa mtoto huyo anatoa harufu kali.Mh.MBUNGE KASSIM MAJALIWA saidi mtoto huyu.anaandika victor katika sura kitabu (Facebook)

anaendelea kuandika Victor IMANI YENU KWANGU IMEMFIKISHA MTOTO RUKIA MAHALI HAPA. NYANGAO- ST.WALBURG'S HOSPITAL
Bila kuchelewa alianza kufanyiwa usafi na mwili wake kupoza harufu mbaya ya awali. hapa akiwa amelowekwa ili maganda yatoke

KADILI MUDA ULIVYOZIDI AKAZIDI KUTIA MATUMAINI.
RUKIA anakunywa sana maji,bila kusita uwa anatamka mwenyewe maji.Muhudumu alisitisha zoezi la usafi na kumpatia maji.
 HAKIKA MUNGU NI MKUBWA RUKIA AKAWA HIVI
Baada ya usafi huu RUKIA akaacha kulalamika,naamini uchafu nao ulikuwa si sehemu ya mateso.
                                                        BABA WA RUKIA APATA FARAJA
Baada ya muhudumu kufanya kazi bila kinyaa wala woga na kubadilisha muonekano wa wa mtoto huyu,alipakatwa na baba yake kwa muda iliawekwe ktk nguo safi.

 Maumivu yenye matumaini ndani yake


RUKIA AMELAZWA WODI NO3 CHUMBA NO2 ST.WALBURG'S HOSPITAL NYANGAO-LINDI TZ. DUA,SALA NA IBADA ZAHITAJIKA SANA KWA MTOTO HUYU.MUNGU AMZIDISHIE PUMZI NA UMRI WA KUISHI HAPA DUNIANI
 HUDUMA ILIZIDI KUIMALIKA KWA MTOTO RUKIA
Hakika Mungu amepenyeza mkono wake ktk shida hii.

Unahitajika msaada wako ili Mtoto huyu azidi kupata nafuu zaidi unaweza kutuma kwa akakunti hizo chini
M PESA 0755 754494
TIGO 0715 754494

1 comment:

  1. kama nchi yetu ingekuwa na utaratibu mzuri mzazi asingekuwa anawaza suala la dawa wala mtoto kwenda hospital
    hii inasababisha serikali kuwa wabinafsi

    ReplyDelete