Pages

Monday, February 13, 2012

DAIMA USIPENDE

Daima usipende kusikiliza habari za watu utajikuta una dhima ya kuwasimulia habari zako,Usimlaumu mtu kukunyima mwaliko katika jambo lake ni dhahiri jambo hilo halikuwa na kheri kwako,usipende kuuliza kila jambo kwani majibu mengine yaweza kuhuzunisha moyo wako,usipende kusimulia furaha yako kwa kila mtu kwani mahasidi hujifanya kufurahi nawe kumbe mioyo yao yawauma,usipende kukaa sana kwa watu kwani kukaa kidogo hudumisha hamu ya kutaka kukuona tena,usimtegemee binadamu mwenzio kwa jambo lolote mtegemee Mola kwa yote kwani binadamu ameumbwa kwa wivu,choyo,chuki na husda...

No comments:

Post a Comment