Pages

Friday, July 31, 2015

KIFUSI KILA BAADA YA MIAKA 5

 Barabara ya mtaa wa mkumba temeke ikiwa inatawanywa kifusi kwa ajili ya vumbi.


Wakiwa wanatawanya kifusi mitaro iko hivi

MUONEKANO WA ENEO LA KITUNDA


Mwonekano wa eneo la kitunda, Mwanagati iliyopo nje kidogo ya jiji la Dar es salaam

Thursday, July 30, 2015

Thursday, July 23, 2015

HII IMEKUAJEEEE! !!


HII INAKUWAJE..................

Hiki ninaweza kuita ni kioja katika moja ya vioja vingi vilivyotokea katika mwaka huu.. hakika inasikitisha sana katika zoezi linaloendelea la uandikishaji la wapiga kura kwa mfumo wa Kielektroniki (Biometric Voters Registration) kuna vitu vya aibu vinafanyika vinavyodhalilisha nchi kuonekana kama kwamba ina uhaba mkubwa wa watu wenye maarifa ya kuweza kutenda kazi.

 kwa mfano; uchukuaji na uwekaji wa picha (pass port) tazama picha iliyowekwa katika hicho kitambulisho hauhitaji kuwa na elimu yoyote kujua hiyo picha haiko sawa na ukichukulia kwamba vitu vya msingi katika kitambulisho ni maelezo (Particulars), saini na picha (Passport size) sasa hiyo picha hapo ni passport, post card au ni kitu gani? Na hiki kitambulisho kinawakilisha vitambulisho vingi (si vyote) vilivyotolewa  katika hili zoezi kwa mtindo huo.Ukiachilia huo utendaji na hata muonekano wa nyuma ya picha (background) ni mbovu haupendezi hata kidogo

Mfano wa umuhimu wa picha angalia pale unapohitaji Hati ya kusafiria (Passport)  unapopewa vigezo ya picha wanayohitaji au hivi ni vigezo tumepewa na wazungu kwa kuwa matumizi ya Pass port ni ulimwenguni kote (worl wide)  na tusipofuata Raia wetu hawataweza kusafiri popote na hiki kitambulisho cha kura kina matumizi ya nyumbani tu basi bora liende..........

 Napenda kuwapongeza wale waandikishaji wa vitambulisho vilivyopita vya Analojia walikuwa na uweledi mkubwa waliweza kuandika (handwriting) na kutoa picha kwa ukubwa unaostahili kuliko hawa wa kidigitali wanaofanya kazi katika kipindi hiki ambao wengine walikuwa hawajahi kukutana na Kompyuta lakini kwa maelekezo na mafunzo ya saa moja tu wanaingia kwenye zoezi kubwa kama hili.

Hivi tatizo ni nini? .................. Au ni wivu unanisumbua!!... naomba niishie hapo niachie wadau kuchangia kwa mustakabali mzuri wa nchi yetu.



Wednesday, July 22, 2015

UANDIKISHAJI WAPIGA KURA TEMEKE



NGOMA AFRICA BAND KUTUMBUIZA INTERN.AFRICAN FESTIVAL TUBINGEN ,JUMAMOSI 25 JULAI 2015


FFU-Ughaibuni Jino kwa Jino na Washabiki wa Tubingen Jumamosi 25,07.2017


Tübingen,Ujerumani

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa Band aka FFU-Ughaibuni yenye makao yake nchini Ujerumani,inatarajiwa kutingisha jukwaa la
maonyesho makubwa ya muziki na utamaduni barani ulaya 6th International African Festival in Tübingen, Ujerumani, bendi hiyo maarufu inayoongozwa na Kamanda Ras Makunja  itapanda jukwaani siku ya Jumamosi 27 Julai 2015 majira saa 2.00 Usiku katika
uwanja wa Festplatz,Europa str,mjini Tübingen ,uliopo Ujerumani ya Kusini. 
Kikosi kazi hiko cha Ngoma Africa Band ukipenda waite viumbe wa ajabu Anunnaki au FFU,chenye utajiri wa wanamuziki vijana waliojaa vipaji, bendi inasadikiwa kuwanasa
washabiki kila kona duniani kutokana na mdundo wake"Bongo Dansi" made in Uswahilini. bendi hiyo kwa sasa inatamba na CD mpya ya " La Mgambo" yenye nyimbo mbili za kumuaga rais JK.
Usikose kuwasikiliza at www.reverbnation.com/