Pages

Sunday, May 31, 2015

NATURE ADHIHIRISHA UKUBWA WAKE

Nature akiweka maiki vizuri ili akamue ipasavyo.
Mashabiki wakimshangilia Nature baada ya kupanda jukwaani.
.…Akikamua kama kawaida yake.
.…Ngoma inaendelea.
Profesa J akiwapa mashabiki kitu walichotaka.
…Akiwaimbisha mashabiki.
....Profesa J akizidi kuzikonga nyoyo za mashabiki.
Snura (katikati) akiwaongoza wanenguaji wake.
Mmoja wa wanenguaji akionyesha machejo.
...Miondoko ya kupagawisha mashabiki ikiendelea.
Shetta akitoa burudani.
…Burudani zikiwa zimepamba moto Dar Live.
DJ Majay akifanya vitu vyake kwenye mashine
SHOO ya kutimiza kutimiza miaka 16 katika muziki kwa msanii Juma Kassim Kiroboto ‘Sir Nature’ na kituo cha Utangazaji cha EFM kutimiza mwaka mmoja iliyofanyika ndani ya ukumbi wa Burudani wa Taifa wa Dar Live, Mbagala-Zakhem, lilikuwa moto wa kuotea mbali.
Katika onyesho hilo Nature, mbali ya kutoa burudani ya nguvu, alipigwa tafu na Snura, Profesa J. Makomandoo, Shetta na Msaga Sumu.

Tuesday, May 19, 2015

NASH MC NA MIAKA 16 YA JUMA NATURE

Hiki ndio alichokisema msanii wa hiphop nchini Nash Mc katika kuelekea miaka 16 ya Juma Nature
Nawapongeza E.FM 93.7 kwa kuandaa Tamasha la miaka 16 katika game ya Sir Juma Nature, hakuna asietambua mchango wa Juma katika kuifikisha sanaa yetu hapa ilipo ukiacha nyota aliyokua nayo ya kupendwa na watanzania wengi, Ni jambo zuri sana na la kuigwa na Media zingine nchini, maana wengi husubiri wasanii wafe watumie mwanya huo kujipatia kipato kwa kuandaa matamasha ya kumkumbuka Hayati huyo,kama ilivyokua kwa Hayati Albert Mangwear, E.FM wamefanya kitu ambacho Alipaswa kufanyiwa Sir Juma Nature muda tu lakini si haba natumai litakua tamasha zuri na kubwa ntajitahidi niwepo siku hiyo kwa kua itakua nyumbani Temeke basi mzukaaaa.
16 Ya Sir Juma Nature katika Game.

KOTA ZA TEMEKE MWISHO YAGEUKA GEREJI BUBU

 Mwonekano wawaneneoalaoKotaa tetemekewMwishoabaadaa gereji bubu uvamia eneo hilo


BARABARA BADO JANGA

 Hii ndio hali halisi ya barabara nyingi temeke kwa kipindi hiki baada ya mvua kukata
 Huu ni mtaa wa temeke sudan Kuelekea Tandika

Mashaka matupu

Monday, May 18, 2015

Matengenezo barabara ya Msimbazi



Barabara ya msimbazi ikiwa katika matengenezo ya kuipanua ili kupisha ujenzi wa mabasi yanayokwenda kasi Dsm.mafundi wakioneka katika hatua za ukarabati wa eneo hilo