Pages

Thursday, April 28, 2011

BAFANA BAFANA vs TANZANIA



The South African Football Association (Safa) and their Tanzanian counterparts reached agreement late on Wednesday to stage an international friendly game at the national Stadium in Dar es Salaam on May 14, it can be confirmed.
Bafana Bafana coach Pitso Mosimane confirmed on Wednesday that he has received confirmation from Safa that the match has indeed been finalised and he will announce his squad to tackle the “Taifa Stars” at the 60 000-seater national stadium on the agreed date.
“I wish to thank Safa and the PSL for their support of our vision,” said Mosimane.
“We have a crucial date with Egypt in Cairo for the African Nations Cup qualifier on June 3 and this will come as a perfect tune-up match for us ahead of that game.
“It goes without saying that if we win that game, we will be in a very good position to qualify for the 2012 Nations Cup in Equatorial Guinea and Gabon. So this Tanzania game is crucial for us in our preparation for that clash and we will take our strongest possible squad for the match.”
Damas Ndumbaro, a Fifa-accredited match agent confirmed that he has finalised the deal with both Tanzanian FA President Leodegar Tenga and Safa CEO Pinky Lehoko for the staging of the match on the above date which has already been submitted to Fifa.
Safa President Kirsten Nematandani also confirmed that Bafana Bafana will play the “Taifa Stars” on the agreed date.
It is not a Fifa date, but the PSL programme will be suspended due to the Nedbank Cup semifinals and Safa seized the opportunity to give the national team much-needed match practice.
Indeed with Kaizer Chiefs, Mamelodi Sundowns and Ajax Cape Town all eliminated from the Nedbank Cup, Mosimane will be able to select most of the players that started against Egypt in the recent Afcon qualifier at Coca-Cola Park.
The country’s number one goalkeeper Itumeleng Khune, teammates Yeye Letsholonyane and Simphiwe Tshabalala, Morgan Gould, Siyanda Xulu, Mzuvukile Tom, Prince Hlela, Eric Mathoho, Thanduyise Khuboni, Siyabonga Sangweni and Katlego Mphela will be available for selection.
In addition, Bernard Parker, who has returned from Greece where he has been playing and is currently training with AmaZulu, will also be available for the showdown against a team that is among the rising countries on the continent.

Wednesday, April 27, 2011

MANISPAA YA TEMEKE

kazi Nzuri kwa wanafunzi wa shule ya Miburani iliyopo Temeke Wailes kata ya Miburani wakionyesha jengo la Manispaa ya Temeke lilivyo
Waliofanya hiyo kazi ni wanafunzi wa kidato cha tatu

Saturday, April 23, 2011

AFA KWA UMEME






mfanyabiashara Bashiru Sebastian (33) amekufa baada ya kunaswa na umeme juzi saa 2:30 usiku katika eneo la Temeke Sudan, Dar es Salaam.

Akielezea ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Misime alisema Bashiru na mwenzake Yasin Shaban (35) walipokuwa wakitokea msikitini juzi, walikuta nguzo ya umeme ya msongo wa megawati 32 imekatika na waya ukining’inia.

Amesema, wakati wakipita karibu na nguzo hiyo, Bashiru alinaswa na kufa papo hapo na Shaban alipojaribu kumnasua mwenzake alipata mshtuko kwenye mguu wa kulia na mkono wa kulia na amelazwa katika Hospitali ya Temeke.

Tuesday, April 12, 2011

WANAONIONEA WIVU WALIE TU-TAMBWE



\Mkuu wa kitengo cha plopaganda wa chama cha mapinduzi Taifa, Tambwe Hizza amesema wanaonionea wivu labda mabadiriko yaliyofanywa katika chama hicho yatanikumba na mimi walie tu kwa kuwa mimi ni muajiliwa.
Akiongea na TEMEKEPAMOJA.BLOGSPOT.COM, Tambwe amesema kuwa mabadiriko katika chama ni ya kawaida na sasa atakuwa akifanya kazi chini ya kijana msomi mwenye upeo mkubwa Nape Nnauye badara ya Chiligati kama ilivyokuwa awali.
Aidha akimzungumzia Katibu Mkuu mpya wa CCM amesema ni mtu muadilifu na mchapakazi na amewahi kukitumikia chama katika nafasi mbalimbali kama mkuu wa itikadi ya uenezi pamoja na kufanyakazi katika sekta mbalimbali Serikalini.
Hata hivyo amekili maumivu yaliyokuwa yakipata chama kutokana na Kashfa za kifisadi "kwa sasa itakuwa imebaki history kwani mwenyekiti wangu ambaye huwa hakulupuki katika kufanya mambo yake ametumia busara na hekima katika mabadiriko hayo" alisema.
Tambwe alitakiwa kutoa maoni yake kuhusu mabadiriko ndani ya CCM hasa nafasi ya katibu Mkuu kutokana na madai kuwa aliwekwa na Mzee Yusuph Makamba kutokana na kuwepo kwa uhusiano wa wote kutoka mtaa mmoja
Hata hivyo Tambwe amekanusha kuwa nafasi hiyo amepewa na aliyekuwa katibu Mkuu wa CCM Taifa Mzee Yusuph Makamba " Hakuna kitu kama hicho bali ni utendaji na uadilifu wangu katika chama ndio ulionifikisha hapa nilipo isiwe dhambi makamba na mimi kutoka katika mkoa mmoja kwani mimi nilikuwa nafanya kazi chini ya Katibu mwenezi John chiligati"alisema huku akionyeshwa kukelwa na maneno hayo.

jahazi wawafunga usher family

WANAMUZIKI wa bendi ya taarab ya jahazi modern taarabu, leo wamewafunga waandaaji wa shughuli za burudani maarufu kwa jina la usher family ya Temeke, katika mchezo wa mpira wa miguu kwa goli moja kwa nunge lililofungwa na kiongozi wa bendi hiyo Mzee Yusuph, mchezo huo uliofanyika katika viwanja vya Luxury pub na kuhudhuliwa na umati wa watu.
Mchezaji Kiboko arambee maarufu kwa jina la HB JAX, itabidi ajutie makosa aliyokuwa akiyafanya katika kipindi cha kwanza dakika ya 27 na kipindi cha pili dakika ya 81 baada ya kupoteza nafasi za wazi alizokuwa akizipata kupitia wingi ya kushoto Dady brown mopao.
hadi dakika tisini zinamalizika jahazi walitoka kifua mbele kwa goli moja kwa nunge
wakati huohuo
Mashindano ya khanga sebene yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Usher family  na kampuni ya Aset Entertiment yaliyokuwa yanawashirikisha wanawake kumi katika kucheza sebene huku wakiwa wamevaa vazi la khanga, yamefikia hatua ya fainali na inatarajia kufanyika siku ya jumapili tarehe 17/04 katika ukumbi wa TCC Chang'ombe jijini Dar es alaam
hadi kufikia hatua hiyo ni wanadada watano ndio waliongia hatua hiyo ya fainali ambapo mshindi wa kwanza anatarajia kuchukua kitita cha Sh 200,000. mshindi wa pili 150,000. na mshindi wa tatu ataibuka na kitita cha 100,000.
mashindano hayo yamedhaminiwa na kampuni ya simu ZANTEL na mkurugenzi wa high way park Hussein Macheni.

CCM MPYA



SEKRETARIETI KUU, Katibu mkuu Wilson Mkama, Mweka Hazina  CCM taifa Mwigulu Lameck Nchemba,Katibu Itikadi Mwenezi wa CCM taifa Nape Moses Mnauye,Katibu Organaizesheni NEC Bi Asha Abdullah Juma,Naibu Katibu mkuu CCM Zanzibar vuai Ali Vuai na January Makamba uhusiano Kimataifa  
            
WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU

Anna Abdalah

Peter Kisumo

Mwigulu Nchemba

Januari Makamba

Aly Juma Shamhuna

Wilson Mukama

Emmanuel Nchimbi.


WANAOINGIA KAMATI KUU

Pindi Chana

Abdulrahman Kinana

Zakhia Hamdan Meghji

Abdalah Kigoda

Steven Wasira

Costansia Buhiye

William Lukuvi

Dk. Hussein Ali Mwinyi

Dk. Maua Daftari

Samia Suluhu

Shanmsi Vuai Nahodha

Omary Yusuf Mzee

Prof. Makame Mbarawa

Mohamed Seif Khatibu     

Monday, April 11, 2011

VYUO VIKUU AFRICA HAVITAMBULIKI



Kuorodhesha vyuo vikuu kulingana na umaarufu ni desturi inayokua kwa kasi sana katika sekta ya elimu ya juu.
Orodha hiyo, inayojumuisha vyuo vikuu vilivyo maarufu zaidi duniani, ina walakini kwani bara zima halimo.
Hutapata hata chuo kimoja kutoka bara la Afrika kwenye orodha hiyo.

Vyuo vikuu vilivyoorodheshwa ni vya Marekani, Ulaya na baadhi kutoka China na Korea Kusini huku Afrika ikiwa imesahaulika.

Mazungumzo yanayohusu utandawazi wa vyuo vikuu yanatumia lugha ya kuvutia iliyorembwa kwa mada ya ushirikiano wa kimataifa, pamoja na mzunguko wa fedha katika mitandao ya kimataifa.

Ni rahisi sana kupotoshwa na mafanikio ya vyuo hivi ambavyo mazoea ni kuwatunukia watu tuzo na kujionyesha.

Swali ni, ikiwa ushindani wa kimataifa wa vyuo hivi utajikita katika hadhi na uwezo wa vyuo vichache, na hivyo basi bara zima likasahaulika, mambo yatakuwa vipi?

Idadi yaongezeka

Kwa mujibu wa taasisi ya takwimu ya shirika la elimu, sayansi, na utamaduni la Umoja wa Mataifa, kuna wanafunzi milioni 4.5 kusini mwa jangwa la Sahara.

Kulingana na orodha hiyo, wanafunzi hawa kutoka bara la Afrika ni kama hawapo.


Bw Thandika Mkandawire

Lakini idadi hii inawakilisha kuwepo kwa ongezeko kubwa. Mwaka 1970, idadi ya wanafunzi Ilikuwa 200,000 katika eneo hilo la Afrika na sasa idadi ya vijana wanaojiunga na chuo kikuu imeongezeka kutoka aslimia moja hadi sita.

Katika takwimu hizi kuna tofauti kubwa zinazojitokeza. Nchini Malawi, takriban asilimia 0.5 ya vijana watajiunga na chuo kikuu wakati Cameroon kiwango kimefikia asilimia tisa.

Pia kuna mienendo tofauti kwa wale wanaoamua kusomea ng'ambo.

Wanafunzi wanaotoka kusini mwa jangwa la Sahara wengi wao husomea nchi za Afrika Kusini na Ufaransa.
Pia wanafunzi kutoka Afrika Kaskazini huenda kusomea Ufaransa.

Tatizo lingine ni kwamba wanawake kutoka bara la Afrika huwa hawajiungi na chuo kikuu kwa wingi.
Ukilinganisha idadi ya wanawake na wanaume katika vyuo vikuu, idadi ya wanaume ndio kubwa zaidi.
Nchini Chad - nchi iliyo kubwa zaidi kushinda nchi za Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zikijumuishwa pamoja - asilimia 0.6 pekee ya wanawake ndio wanaojiunga na chuo kikuu.

Ingawa idadi ya wanafunzi kuongezeka barani Afrika ni jambo zuri, hii itaathiri mambo mengine pia.
Kwa mujibu wa Benki Kuu ya Dunia, ongezeko la idadi ya wanaojiunga na chuo kikuu imeongezeka mno hata kuzidi uwezo wa kifedha wa vyuo hivyo kuajiri wafanyakazi na kununua vifaa.

Mwelekeo tofauti wa ufadhili

Profesa Thandika Mkandawire, mkufunzi wa maendeleo barani Afrika 'African Development' katika chuo kikuu cha LSE alisema, vyuo vikuu vya Afrika bado vinajaribu kurudi katika hali yake kutokana na kukosa ufadhili miaka ya 80 baada ya fedha hizo kuhamishwa kwenye shule za msingi.

Katika enzi za baada ya ukoloni kwenye miaka ya 60 na 70, vyuo vikuu vingi viliibuka barani Afrika lakini hali hii ilisitishwa ghafla. Na wakati maeneo mengine duniani yalikuwa yakiwekeza kwenye elimu ya juu, bara la Afrika lilikosa fursa hiyo.

Profesa Mkandawire alisema "Ukishaangamiza chuo kikuu, ustawishaji wa chuo hicho tena utakuwa si rahisi."


Waandamanaji wadai uwekezaji kwenye elimu

Huenda itakuwa vigumu sana kujaribu kukaribia vipimo vya maendeleo vilivyoko katika vyuo vikuu vingine duniani baada ya 'miaka mingi' iliyopotezwa.

Prof Mkandawire alisema, watu wenye kipato cha kawaida wanajitahidi kushinikiza kuwepo kwa vyuo bora zaidi ili ijadiliwe kwenye duru za kisiasa.

Pia kuna ufahamu kuwa vyuo vikuu ni sekta mojawapo iliyo muhimu katika kuujenga uchumi wa kisasa.
Jo Beall, makamu mkuu wa chuo kikuu cha Cape Town Afrika Kusini (chuo pekee kutoka Afrika kuwa miongoni mwa vyuo vikuu 200 vilivyo bora) alisema "Vyuo vikuu ndio pahala panapo fursa ya kujipandisha katika tabaka za kijamii."

Rasilimali yaadimika

Bi Beall alielezea jinsi alivyoona barabara za kuelekea chuo kikuu kimoja Afrika ya kati zikiwa zimejaa foleni za watu wakiwa na mashine ya kupiga chapa ili kutoa huduma kwa wanafunzi, zikiwa zinaendesha na betri za gari, wakiwa wananakili vitabu vya miaka ya 50.

Wanafunzi hulazimika kusafiri kwa saa tatu au nne ili kufika chuo kikuu.


Wasiwasi wa kisiasa umekuwa kikwazo kwa uwekezaji barani Afrika. 

Isitoshe, ukumbi wa mihadhara hujaa kupindukia hadi kuna walinzi na lango la kudhibiti msongamano wa watu.

Profesa Beall ambaye atajiunga na taasisi ya 'British Council' baadaye mwaka huu alisema, licha ya hayo, bado ana matumaini kuhusu mustakabali wa mfumo wa elimu ya juu Afrika.

Kuna vyuo vikuu vinavyojitahidi kuwa taasisi zinazojishughulisha na utafiti wa hali ya juu.
Phillp Altbach, mkurugenzi wa 'Centre for International Higher Education Boston College' Marekani alisema udhaifu wa vyuo vikuu barani Afrika haitokani tu na ukosefu wa fedha bali kuna kasoro kadha wa kadha ikiwa ni pamoja na msukosuko wa kisiasa na ubadhirifu wa mali.

Kushindwa kuvutia

Soko la wanafunzi kutoka nje halijafanikiwa kuwavutia wanafunzi kwenda barani Afrika. Badala yake, wasomi wamelihama bara hilo kwenda kuishi ng'ambo.

Chuo kikuu Tunis

Vyuo vikuu vya Marekani na Uingereza vimewekeza katika matawi ya vyuo vyao barani Asia na Mashariki ya kati badala ya Afrika.

Pia Afrika, ambapo utajiri mkubwa sana na umaskini uliokithiri, umekosa watu wenye uwezo wa wastani Afrika hawana ushawishi kama wale wanaoishi nchi za China na India ambako wamechochea ustawishaji wa elimu ya juu nchini mwao.

Pamoja na uwekezaji wa fedha, alisema kunahitajika mabadiliko ya kitamaduni kama vile kulinda uhuru wa kitaaluma ili kuweka hali itakayoimarisha vyuo vikuu.

Lakini hakuna kuepuka pengo la kiuchumi.

Aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Blair ameunda wakfu inayofanya kazi na mtandao wa vyuo vikuu duniani kote, ikiwemo Afrika na Marekani.

Alisema chuo kikuu cha Yale, Marekani si tu kwamba kina uwezo mkubwa kifedha na chuo kama cha Fourah Bay College Sierra Leone - mali iliyowekwa wakfu ya Yale ni mara chungu nzima zaidi ya utajiri wa nchi nzima.

Ruth Turner mkurugezi mkuu wa wakfu hiyo alisema tofauti hii illiopo kwa sasa haitokani na hali ya uchumi tu bali kunahitajika kuliangalia suala hili kwa misingi ya maadili.
"Sote tunaishi katika dunia ya utandawazi lakini tunakosa namna ya kujadili tatizo hili tukizingatia maadili."

Maendeleo ya kiuchumi

Katika utandawazi duniani, vyuo vikuu vyenye uwezo vinaonekana kunufaika zaidi na vile vilivyo maarufu zaidi.

Chuo kikuu cha Free State

Vyuo vikuu vilivyo katika mstari wa mbele ni "taasisi za kimataifa. Vyuo hivi vinaweza kuwavutia wakufunzi waliobobea na vina uhusiano na sekta ya biashara pamoja na kuwa na ushawishi uliovuka mipaka" alisema Keith Harman ambaye anafanya kazi kwenye mradi unaofadhiliwa na jumuiya ya madola kuendeleza vyuo vikuu nchini Uganda ili kuwavutia wanafunzi wa Afrika mashariki na kusini.

Kwa upande mwingine, vyuo vikuu vingi barani Afrika ambavyo havina uhusiano kama huo "manufaa ya utandawazi "
"Vyuo vikuu ni misingi muhimu ya kuwaleta watu waliostadi na pia vina umuhimu katika kuleta maendeleo ya kiuchumi" alisema Bw Harman lakini vyuo vingi Afrika vinapoteza fursa ya kupanda daraja kwani havijafanikiwa katka uwekezaji na utafiti zaidi, pamoja na uwezo wa kuwavutia wanafunzi kutoka ng'ambo.
Profesa Makandawire alisema hata hivyo, kuna dalili za kuwepo na matumaini. " Kuna mabadiliko, mambo yanakuwa wazi zaidi ; ukandamizaji umepungua."

Alisema pia kuna ufahamu kuwa kusitisha uwekezaji katika vyuo vikuu ilikuwa ni makosa ambayo sasa yanarekebishwa.

Aliongezea "Kuna matokeo mazuri ambayo yanayojitokeza" lakini alitoa ilani kuwa maendeleo yatachukua miaka mingi ya kazi ngumu.

BBC

APIGWA MOTO BAADA YA KURUKA UKUTA





Pius Micky wa blogu ya Spoti Starehe anafahamisha kupitia blogu yake na ukurasa wa Facebook kuwa, kijana mmoja kwa jina Lilah Hussen (pichani) amechomwa na moto mwili mzima na walinzi wa Hotel ya South Beach wakishirikiana na Meneja mmiliki wa Hotel hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Shipata.

Wakiongea na kamera ya Spoti Starehe, ndugu wa majeruhi huyu wamesema kuwa ndugu yao alifika ufukweni hapo ambapo kila mwisho mwa wiki panakuwa na muziki kwa ajili ya kujiburudisha na alipoingia ndipo alipokamatwa na walinzi kwa kutokuwa na alama maalumu ambayo huvaliwa mkononi kwa waliolipa kiingilio (kiingilio ni Tsh. 7000/- kwa mtu) ndipo walipompeleka kwa Meneja wa Hoteli hiyo na aliamrisha kijana huyo avishwe mpira na kuchomwa moto.

Bwana Lila ambaye kwa sasa emehamishiwa Hospitali ya Rufaa Muhimbili amesema yeye ni mfanyabiashara ndogo ndogo na mkazi wa Kigamboni na kuwa alikwenda hapo baada ya kuvutiwa na muziki pasipo kujua hayo yangemkuta.

Ndugu wa majeruhi huyu wamefungua kesi katika kituo cha Polisi Kigamboni lakini kwa masikitiko wanasema bado si uongozi wala walinzi wameshakamatwa.

Ufukwe wa South Beach unajizolea umaarufu kwa michezo ya ufukweni lakini wananchi wa kawaida ambao wanaishi eneo hili wamekuwa wakilalamikia ada kubwa ya kiingilio ufukweni hapo ikiwa ni Tsh. 7000/- ada ya kuingia tu bila kinywaji.

credit : Pius Micky/Spoti Starehe blog

Serikali ya Gaddafi yakubali mpango wa amani,asema Zuma

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma anasema serikali ya Libya imekubali mpango wa amani wa muungano wa Afrika ili kumaliza mapigano ya miezi miwili.
Bwana Zuma na viongozi wengine watatu wa Afrika walikutana na kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi, mjini Tripoli siku ya Jumapili.Sasa wanaelekea katika eneo la Benghazi linalodhibitiwa na waasi mashariki mwa nchi.
Katika eneo la Ajdabiya,vikosi vinavyomuunga mkono Gaddafi vimewazidi nguvu waasi katika mapigano.
Shirika la Nato linasema ndege zake zimeshambulia vifaru 25 vya serikali katika siku ya Jumapili pekee.
Mpango wa muungano wa Afrika unatoa wito wa kusitishwa kwa mapigano mara moja, kufunguliwa njia kwa ajili ya kusafirisha misaada na mazungumzo kufanyika kati ya serikali na waasi.

"muhimu kusitisha mapigano," alisema rais Zuma,baada ya mazungumzo yaliyochukua saa kadhaa.
Mfumo ambao mchakato huo utachukua mtaelezwa baadaye katika taarifa zetu,alisema Bwana Zuma.
Mwakilishi wa upinzani aliye Uingereza, Guma al-Gamaty,akizungumza na BBC amesema kuwa wataangalia kwa makini mpango huo wa muungano wa Afrika,lakini mpango wowote ulio na nia ya kumuacha Gaddafi au wanawe madarakani hautokubalika.

Gbagbo akamatwa baada ya purukushani

Laurent Gbagbo akionyeshwa kwenye televisheni muda mfupi baada ya kukamatwa

Kiongozi wa Ivory Coast Laurent Gbagbo ametiwa kizuizini mjini Abidjan na kuwekwa chini ya ulinzi wa polisi wa Umoja wa Mataifa.

Alikamatwa wakati majeshi ya kiongozi anayetambulika kimataifa kuwa Rais wa nchi hiyo Alassane Ouattara na vifaru vya Ufaransa kuingia kwenye makazi yake.

Bw Gbagbo alikuwa akikataa kukabidhi madaraka, akisema alishinda uchaguzi wa Rais wa mwezi Novemba.
Ufaransa ilisema majeshi yanayomwuunga mkono Ouattara yalimkamata, lakini washirika wa Bw Gbagbo walisema ni majeshi maalum ya Ufaransa.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon alisema kukamatwa kwa Bw Gbagbo kumemaliza miezi kadhaa ya ghasia zisizo na sababu, na Umoja wa Mataifa utaunga mkono serikali mpya.
Majeshi ya kutunza amani ya umoja huo yaliyashutumu majeshi yanayomwuunga mkono Bw Gbagbo kwa kuhatarisha maisha ya raia na kuiomba Ufaransa, ambalo lilikuwa koloni lake, kuondosha silaha nzito za kiongozi huyo.

Kumekuwa na madai ya ukatili kufanywa na wote wafuasi wa Gbagbo na Ouattara, na umoja huo una taarifa ya zaidi ya watu 1,000 kuuawa na takriban 100,000 kukimbia nchi hiyo.
Wawakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa wa Ivory Coast, Youssoufou Bamba, walisema Bw Gbagbo atashtakiwa.

Mjini London, Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague alisema kama atafunguliwa mashtaka, basi ashtakiwe kwa kuzingatia njia zinazostahili.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton alisema mjini Washington kwamba kukamatwa kwa Bw Gbagbo kumepeleka ujumbe kwa "madikteta" ambao "hawatopuuza sauti za watu wao katika uchaguzi wa haki na huru."

Saturday, April 9, 2011

HITMA YA FIVE STAR



Kwanza kabisa ningependa kukufahamisha  kuwa imeundwa kamati ya kusimamia kisomo cha wasanii wa Five Star Modern Taarab waliofariki katika ajali iliyotokea Jumatatu 21/03/2011 Mkoani Morogoro.

Kamati hiyo itakuwa chini ya Mwenyekiti Mh. Abbas Mtemvu (Mbunge wa Temeke), Makamu Mwenyekiti: Sheikh Omar Alhadi ( Naibu Imamu msikiti wa kichangani), Katibu: Saidi Mdoe (Mkurugenzi Screen Masters) Mweka hazina ni Ashraf Ahmed (Mkurugenzi wa fedha East African Melody)

Kamati hii ina jumla ya wajumbe 14 wakiwemo Idd Azan (Mbunge wa Kinondoni) Mh. Azan Zungu(Mbunge wa Ilala na wengineo wengi.

Kamati hii kwa kushirikiana na uongozi wa Five Star umeamua kufanya hitma kubwa yenye sura ya kitaifa siku ya Jumapili 17/04/2011 katika ukumbi wa PTA sabasaba.

Ili kufanikisha shughuli hii ukiwa kama mdau wa sanaa hapa nchini, kamati inaomba mchango wako wa hali na mali

Tunaomba uwasilishe mchango wako kwa mweka hazina (Ashraf Ahmed 0713232747) au kwa katibu Saidi Mdoe( 0713 606109) kabla ya terehe 10/04/2011 na utapatiwa stakabadhi ya kuthibitisha mchango wako kupokelewa.

Said Mdoe
Katibu

Friday, April 8, 2011

KATIBA MPYA CHINI YA SAA 100!


Ndugu Zangu,


TUMEONA na kusikia kwenye taarifa ya habari TBC1 jana usiku, Waziri wa Sheria Na Katiba Bibi Celina Kombani akitamka; kuwa utaratibu wa kukusanya mawazo ya wadau juu ya mapendekezo ya Muswaada wa Sheria itakayosimamia mchakato wa kupatikana kwa Katiba Mpya utachukua siku tatu!


Na ulianza jana, Dodoma na Dar es Salaam. Leo zimekuja taarifa, imeongezwa siku moja zaidi. Utachukua siku nne, saa 96. Naam. Chini ya saa 100! Ina maana , kuwa baada ya saa 96 za kukusanya maoni ya wadau Muswaada utarudi tena bungeni na kujadiliwa na waheshimiwa wabunge.



Na ukipitishwa, basi, mchakato unaendelea ukimruhusu Rais kuanzisha mchakato kwa kuwateua wajumbe wa Kamati itakayoratibu mchakato na mengineyo. Na tafsiri kuu hapa ni hii; Watanzania tutakuwa tumepewa Katiba Mpya tunayoililia chini ya saa 100. Na lifuatalo nina hakika nalo, kuwa Watanzania HATUTARIDHIKA nayo. Kwanini? Fuatilia ninachoandika, utanielewa.


Ni juzi tu nimeandika kupitia safu yangu kwenye Raia Mwema, kuwa; ” Nauona, mwelekeo mbaya wa upepo wa kisiasa nchini mwetu. Nina shaka kubwa. Naamini, tuko wengi wenye mashaka na mwelekeo wa nchi yetu tunayoipenda.” ( Mraba Wa Maggid, Raia Mwema, Aprili 6, 2011 )


Kwenye makala yangu ile niliweka wazi, kuwa katika hili la mchakato wa kupata Katiba Mpya tumeanza na mguu mbaya. Tumeyaona Dodoma na Dar es Salaam jana. Sikuhitaji kuwa na Elimu ya Unajimu kubaini hilo. Tulishaziona ishara.


Hakika, ikitaka, Serikali inaweza kurudi nyuma na kuanza upya. Wahenga walitwambia, ni heri nusu shari kuliko shari kamili. Katiba ni ya Watanzania, kwanini usiwepo ’ Mchakato Kivuli’- Shadow process utakayojumuisha makundi mbali mbali ya kijamii. Wajadili kwa uhuru kabisa, yote. Kisha nao waje na mapendekezo yao. Ingeepusha shari kamili.


Haiyumkini suala nyeti kama la Muswaada wa Mapendekezo ya Sheria itakayosimamia mchakato wa Katiba likajadiliwa na wadau kwa siku nne tu. Ndio, chini ya saa 100. Maana, Katiba ya nchi ni kitabu nyeti chenye kuhusu maisha ya kila siku ya Mtanzania. Hauingii akilini, utaratibu wa wadau kujadili Muswaada huu kwenye kumbi za Msekwa Dodoma na Karimjee Dar. Halafu ikawa basi, imetosha. Urudishwe kwa Wabunge, waujadili, kisha waupigie kura, na zaidi kuupitisha.


Watanzania tuko zaidi ya milioni 42. Ni vema na ni busara kukawepo na wigo mpana zaidi wa kuwafikia Watanzania wengi zaidi kadri inavyowezekana. Hivi, inatoka wapi, ’ghafla’ na ’dharura’ hii ya wadau kutakiwa kutoa maoni yao ndani ya saa 96? Maana, hili ni suala nyeti kwa Watanzania na lenye kuhusu mustakabali wa nchi. Kwa nini tusipewe muda zaidi wa kutafakari?


Na wahusika wana nafasi ya kujisahihisha na kuokoa sura zao. Maana, tukubali, kuwa mchakato unaoendelea hautasaidia kupata Katiba itakayowapa imani Watanzania kuwa italinda maslahi ya taifa lao na yenye kukidhi matakwa ya wakati tulionao. Hayo ni mashaka ya kweli ya Watanzania walio wengi, yasipuuzwe. Na Watanzania wanajua, kuwa wanachokitafuta sasa walikuwa nacho, walikipoteza, kwa bahati mbaya.


Na kuna kisa kutoka Uganda. Milton Obote, mbali ya mambo mengine, anakumbukwa na Waganda kwa tukio la kihistoria la ’ Kuchakachua’ Katiba ya nchi hiyo kwa kuifanyia mabadiliko kinyemela. Ilikuwa Aprili 15, 1966. Ilikuwa aubuhi moja. Wabunge wa Uganda, kabla ya kikao, walielekezwa kwenye masanduku yao ya makabrasha bungeni wakachukue ’ Muswaada wa dharura’ wa Marekebisho ya Katiba.



Muswaada ule wa Marekebisho ya Katiba ukajadiliwa ’ kishabiki’ na kupitishwa ndani ya saa moja. Unakumbukwa kwa jina maarufu la ’ Pigeon-hole’ Constitution- Katiba ya Sanduku la Makabrasha. Ni kitendo kile cha Obote, ndicho kilichopelekea Uganda kupitia wakati mgumu kwa miaka miaka mingi zaidi baadae.


Si tunajua, kuwa Obote alikuwa na ugomvi na chama cha KY- Kabaka Yekka. Hivyo basi, alikuwa na ugomvi na Mfalme Fredrick Kabaka na WaBaganda. Katiba mpya ikampa nguvu nyingi Obote na UPC yake- Chama chake. Kabaka na WaBaganda walimtambua haswa Obote. Aliwanyanyasa kwa kuwafunga na hata kuwaua. Ndio, aliwanyamazisha, kwa muda.


Lakini naye, Obote, hakubaki salama. Idi Amin akaja akampindua na kushangiliwa sana na WaBaganda wa Kampala na kwengineko. Kosa alilofanya Obote ni hili; kubadilisha Katiba kukidhi mahitaji yake na ya Chama chake katika wakati uliokuwepo. Obote hakuiangalia Uganda ya miaka 50 hadi 100 iliyofuata. Na hilo ndilo tatizo la viongozi wetu wengi Afrika.


Tukirudi hapa kwetu, kwa kuusoma Muswaada ule wa sheria inatoa tafsiri hii; kuwa ndani ya saa 96 zilizopangwa za kupokea maoni ya wadau zitakuwa zimeweka msingi wa Watanzania kupatiwa Katiba Mpya wasiyoitaka, lakini, itakuwa imehalalishwa, kwa taratibu za Kibunge.



Kwani, haitarajiwi Wabunge wa CCM walio wengi kuukwamisha Muswaada huo. Na ikitokea wakafanya hivyo, kwa maana ya Wabunge hao wa CCM wakaukwamisha Muswaada huo wa sheria, basi, Wabunge hao wa CCM watakuwa wameanza kazi ya ’ Chama kujivua magamba’ na baadhi yao kunusurika na adhabu ya wapiga kura ifikapo 2015.


Ni ukweli, kuwa Nchi yetu iko njia panda. Mbele yetu kuna njia mbili; moja inaelekea tunakopita sasa. Kwenye hali ya ’ kujifunga’ na kubaki tulipo bila kupiga hatua za haraka za maendeleo huku baadhi, wakiwamo viongozi, wakiwa na udhibiti mkubwa wa hali ya mambo. Njia nyingine inaelekea kwenye uhuru zaidi wa wananchi na uwezo wa kuwadhibiti na kuwawajibisha viongozi wao. Ni njia inayoelekea kwenye ustawi wa nchi.

Watanzania tuna kiu kubwa ya kuianza safari ya kuipita njia ya pili. Njia yenye uhuru zaidi na matumaini ya ustawi wa taifa. Njia itakayotufanya tuondokane kabisa na njia ya kwanza, njia inayotufunga na kutubakisha hapa tulipo.
Kwa viongozi watakaochangia kutupitisha kwenye njia ya kwanza, nahofia, kuwa hao watakumbukwa kwa dhamira yao hiyo mbaya kwa Watanzania.


Kwa wale viongozi watakaochangia katika kutupitisha kwenye njia ya pili, basi, hao hawatasahaulika mioyoni mwa Watanzania. Watakuwa ni wanadamu walioamua kuachana na ubinafsi na kutanguliza maslahi ya taifa. Ni imani yetu, kuwa hata Wabunge wengi wa CCM wanaweza kuingia katika kundi la viongozi hao. Kutupitisha kwenye njia ya pili.


Na kama Bunge letu litabariki azma ya Serikali kuendelea kutupitisha katika njia hii ya kwanza kwenye mchakato huu wa Katiba, basi, ni dhahiri, kuwa tuendako kuna giza zaidi kulipo hapa tulipoanzia. Kuna watakaoikumbuka Katiba yetu ya sasa.


Na hiki ni kipindi kigumu sana Nchi yetu inakipitia tangu tupate Uhuru wetu.
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.


Maggid,
Dar es Salaam
Ijumaa, Aprili 8, 2011

Monday, April 4, 2011

BLACK MAMBA IS ABOUT TO STRIKE-TAKE HOME MASSAGE


I wouldn't be able to confirm who wrote this for sure, but I can surely tell you, it has a message to take home, well, that is, if you really care. Got into my inbox from a friend.

‘A special message for the parents & parents-to-be’

Children are a photocopy of their parents's character
You are the hydro power dams from which they
Can tap the power of living light.
But if the dams are empty of values, and the water levels are too low,
What will they tap? Only darkness.
Many parents are suffering from T.B, Too Busy!

Yes, the cost of living is high, but ,the cost of loving is affordable.
 
Each child is a goldmine and it’s the parents to mine the gold out of them;
Sarcastically, there are parents who see their children as a form of tax;
Tax on their time, tax on their comfort and tax on their freedom  and immediately send them to boarding school even in nursery, so as to evade these taxes.
Remember, children are like the Global Fund, a gift and a donor fund from God,
You will have to provide full accountability for their use or mismanagement,
You shall be audited!
 
The home is the first classroom in which a child sits.
But unfortunately, the teachers i.e. the parents, have absconded from duty
And if you ask them, they will tell you,
To them, TV is their daddy, they see him everyday;
The radio is their mummy; she talks to them whenever they want;
Parents, these are your children and, have boarded the wrong taxis, to the Northern bypass of destruction.
 
Physically, they maybe in University, but mentally, they are in kindergarten
With their minds still wrapped up in nappies.
Don’t just be the head of the home but head the home

Forget not, PARENT means;
P – Personal Friend,
A – Available,
R – Responsible,
E -  Encourages
N – Nurtures and
T – Teaches

Now is the time for IDPs (Internally Displaced Parents) to return home,
So that the reconstruction of the family can begin.
There are parents who are living in camps of bondage called bars;
Extramarital affairs, cross generational rapports…..
They need to come home for the family is under attack
 
Many homes used to be like Celtel, Making Life Better,
But now, they have become like Baghdad, daily explosions of verbal artillery,
All this detonated by marital conflicts!
You the parents, have become suicide bombers, blowing up our future,
When we see daddy approaching, ‘black mamba is about to strike’; We take cover as he comes heavily armed with words of mass destruction.
Other parents are like UMEME, they load shed their time for their children,
Even up to one week and the kids end up in a black out of values.
The lucky ones survive if they have friends, who act as generators, providing insufficient power.
 
The parliament and cabinet are the brain of the government.
But the family is the foot of the nation.
When it fails to stand, the nation falls
Parents, have time for your children.

Say, ‘NEVER AGAIN’.
http://www.wavuti.com

Sunday, April 3, 2011

SIMBA SC 2 - TP MAZEMBE 3

moja ya hatari katika goli la simba
ujumbe wa Mechi


Washabiki wa TP Mazembe

Goli la pili la simba Mbwana Samatta akishangilia